YoungConciousâ„¢

Be Updated on the World of Sports, latest News and Entertainment Stories.

Propellerads

Breaking News

Translate

Welcome to Young concious .blogspot.com ==>>Feel free to leave your comment

Jumapili, 21 Mei 2017

China:Marufuku Uuzaji wa nyama ya Mbwa

Marufuku ya uuzaji wa nyama ya mbwa yazuia wasiwasi katika hafla ya Yulin China
Marufuku ya uuzaji wa nyama ya mbwa yazuia wasiwasi katika hafla ya Yulin China

Sherehe ya kula nyama ya mbwa nchini China ilio na umaarufu kwa ukatili wa wanyama mwaka huu itapigwa marufuku kuuza nyama ya mbwa.
Ulaji wa mbwa nchini China sio haramu na wauzaji wa nyama hiyo tayari wameanza kulalamikia marufuku hiyo wengine wakisema hawajaisikia .
Sherehe hiyo inayofanyika mwezi Juni kila mwaka imekuwa ikivutia pingamizi kubwa kutoka kwa wanaharaki wa wanyama wanaosema kuwa wanyama hao hufanyiwa ukatili.
Inakadiriwa kuwa katika sherehe hiyo ya Yulin iliofanyika miaka michache iliopita, takriban mbwa na paka 10,000 walichinjwa na kufanywa kitoweo wakati wa sherehe hiyo ya siku kumi.
Lakini idadi hiyo imekuwa ikipungua katika siku za hivi karibuni huku pingamizi ikiendelea nchini China na kimataifa.
Wanaharakati kadhaa wa wanyama wanasema kuwa wauzaji na mikahawa wameambiwa kwamba hakuna nyama ya mbwa itakayouzwa wakati na kabla ya sherehe hiyo.
Peter Li, mtaalamu wa sera za China aliambia BBC kwamba mamlaka tayari imejaribu kuwakatisha tamaa wanaotekeleza hatua hiyo ,na kwamba mwaka huu itawapiga faini watakaokiuka marufuku hiyo.
 
Raia wa China wakila nyama ya mbwa wakati wa sherehe ya Ylin nchini humo
Raia wa China wakila nyama ya mbwa wakati wa sherehe ya Ylin nchini humo
Sheria hiyo itaathiri wauzaji wa nyama ya mbwa, wafanyibiashara na wenye mikahawa.
Lakini marufuku hiyo itakuwa ya muda ikimaanisha kwamba mbwa wengi wanaweza kuchinjwa kabala ya sherehe hiyo.
''Bado kuna pingamizi kutoka kwa wafanyibiashara wa nyama hiyo ya mbwa'', alisema bwana Li.
''Kote nchini walikuza ulaji wa nyama ya mbwa kama utamaduni wa kitaifa pamoja na chakula cha Wachina.
Hilo sio la kweli ,baraza la mji wa Yulin haliweza kufanya kitu kama hicho kwa kuwa kitasababisha wasiwasi mkubwa kwa kijamii.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Propellerads