
Mabibi
na Mabwana…… kwa mara nyingine tena Ay ambaye ni msanii wa Tanzania
amerudi kwenye headlines za kuruka kimataifa baada ya zile ahadi kutimia
za kufanya single pamoja na staa wa dunia Sean Kingston.
Niliwahi kumsikia akiongea zaidi ya mara nne kwamba kolabo hii
ingefanyika lakini haikuwa hivyo kutokana na sababu ambazo zilizokuwa
nje ya mipaka yake ambapo bila kukata tamaa, Ay ameweza kuvumilia kwa
miaka yote hii toka alipoahidiwa na Sean aliekuja Tanzania mwaka 2010.

Ay alishawahi kuipa nafasi
millardayo.com
kusikiliza single aliyoifanya na Sean Kingston zaidi ya mwaka mmoja na
nusu uliopita lakini alichelewa kuitoa sababu hakutaka kuitoa bila video
hivyo baada ya ratiba za Sean kukaa vizuri ndio wameingia mzigoni.
Source:
MillardAyo
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni