YoungConciousâ„¢

Be Updated on the World of Sports, latest News and Entertainment Stories.

Propellerads

Breaking News

Translate

Welcome to Young concious .blogspot.com ==>>Feel free to leave your comment

Jumanne, 17 Desemba 2013

Ratiba ya 16 UEFA hii hapa.



16 bora
Ratiba ya hatua ya 16 bora ya ligi ya mabingwa barani ulaya imepangwa hii leo huko Nyon nchini Uswissi yalipo makao makuu ya shirikisho la soka barani ulaya .
Ratiba hiyo inaonyesha kuwa Mabingwa watetezi Bayern Munich watacheza na Arsenal , timu iliyofika fainali msimu uliopita ya Borrusia Dortmund itakipiga dhidi ya Zenith St Petersburg toka Urusi .
Michezo mingine itazikutanisha Chelsea ya England na Galatasaray katika mchezo ambao utawakutanisha Kocha Jose Mourinho na wachezaji wake wa zamani Wesley Sneijder na Didier Drogba . Manchester United watacheza na Olympiakos ya Ugiriki huku Real Madrid wakicheza na Schalke 04.
Mabingwa zamani Fc Barcelona watacheza na Manchester City , Ac Milan watacheza na Atletico Madrid huku Paris St Germain wakicheza na Bayer Leverkusen.
Michezo hiyo itapigwa kuanzia tarehe 18 , 19 , 25 na 26  mwezi Februari huku marudiano yakichezwa mwezi machi tarehe 12 , 13 , 18 na 19.

Arsenal vs Bayern Munich
Ac Milan vs Atletico Madrid
Galatsaray vs Chelsea
Manchester City vs Fc Barcelona
Bayer Leverkusen vs Paris St Germain
Schalke 04 vs Real Madrid
Olympiakos vs Manchester United.
Zenith St Petersburg vs Borrusia Dortmund.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Propellerads