Ndio utajiuliza ilikuaje mpaka jamaa akaiba gari la Polisi kwenye mazingira haya.
So inaelekea wizi wa magari unaweza kuwa ‘kipaji’ kwa hawa ndugu zetu wa Afrika Kusini manake kuna kijana mmoja wa miaka 19 huko Northern Cape alifanya kitendo cha kujiamini zaidi pale alipoiba gari la Polisi, yaani ingekua ni gari binafsi linalomilikiwa na askari ingekua afadhali ila hili aliloiba ni gari la Polisi kabisa na nembo zake.
Ilikuaje mpaka akafanikiwa kuliiba? ……alipata hiyo nafasi baada ya Polisi kwenda kwenye eneo la tukio kulikotokea ajali kwa hiyo baada ya Polisi wote kushuka huku funguo za gari zikiwa zimeachwa sehemu yake ndio jamaa akapiga gia.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni