Mashuhuda
wanasema hii nyumba ndiko wamehamia wageni ambapo wakati wa zoezi la
utoaji na uchomaji taka ndiyo bomu likakutwa jalalani.
Kwa mujibu wa maelezo ya mashuhuda, saa moja na dakika 45 usiku Wanajeshi walifika kwenye eneo hilo na kulikagua na kusema lile halikua bomu la kawaida, ni kombora ambalo lilitegwa miezi miwili iliyopita na lilikua tayari kulipuliwa ambapo kama lingelipuka lingeweza kuathiri eneo kubwa sababu ya nguvu yake kubwa.
Eneo lilikokutwa bomu hili ni Kijitonyama Dar es salaam karibu na kanisa la KKKT ambapo wakati huu tunasubiria maelezo ya Polisi, tumeyakusanya hayo yote hapo juu ambayo yametolewa na mashuhuda.
Source: MillardAyo

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni