Kuhusu mtandao wa twitter kufungiwa Uturuki.
Sababu iliyotolewa juu ya kitendo hicho kutoka kwa ofisi ya waziri mkuu ni kwamba kuna ongezeko la kesi za wananchi wa Uturuki kuhusiana na twitter kila siku na kuna uwezekano sababu yenyewe hasa ikawa ni tofauti kwasababu Erdogan amekua akikasirishwa na uvujaji wa rekodi za mazungumzo yake ya simu kwenye mtandao huo.
Amezungumza na familia, Wanachama wa baraza la mawaziri, Waandishi wa habari na mazungumzo ya kibiashara pia malalamiko ya utumiaji wa rushwa juu yake ambapo hii imeanza tangu Disemba 17 2013 wakati ufisadi ulianza kutambulika katika nchi hiyo na kusababisha kujiuzulu kwa Mawaziri wanne mpaka sasa.
Wakati Uturuki inaelekea kwenye uchaguzi march 30, Erdogan na wasaidizi wake wa karibu wamekuwa wakiogopa kutokezea kwa uvujaji wa habari za ndani ambao utaweza kuathiri cheo cha chama tawala .
Hakukua na mategemeo ya yeye kuchukua sheria ya kufunga mtandao wa kijamii wa twitter haraka kama alivyofanywa lakini pia saa kadhaa baada ya kufungwa na kupigwa marufuku kwa mtandao huo, wananchi wa Uturuki wameweza kurudi twitter kupitia teknolojia ya digital.
Kati ya raia waliorudi twitter baada ya kufungwa huko kwa mtandao ni naibu waziri mkuu Bulet Arinc na Meya Melih Gökçek wa nchi hiyo ambae anafahamika kuwa mtumiaji mkubwa wa mtandao huo.
Dosey aliretweet post iliyotumwa na twitter’s global policy team ( timu ya sera za uma za kimataifa ya twitter) iliyosema watumiaji hao watumie ujumbe kwa kuanza na neon START na kutuma kwenda namba 2444, pamoja na 255.
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni