YoungConcious™

Be Updated on the World of Sports, latest News and Entertainment Stories.

Propellerads

Breaking News

Translate

Welcome to Young concious .blogspot.com ==>>Feel free to leave your comment

Alhamisi, 28 Novemba 2013

#Fahamu: Malkia Kassu mshindi wa taji la “Miss Commonwealth Africa”

Malkia Kassu mshindi wa taji la “Miss Commonwealth Africa” apongezwa na ubalozi wa Tanzania Uingereza

The crowned queens of the Commonwealth 2013-pic by Jay Pedram

Mtanzania, Malkia Kassu ( wa tatu toka kushoto) akiwa na washindi wenzake – wote wamevalia taji na kubeba vikombe vya ushindi.
Mashindano ya 2013 yalikuwa mjini London Jumamosi Novemba 16 na  kwa mara ya kwanza yalikuwa na mshiriki toka  Tanzania.
Malkia Kassu (  jina la kuzaliwa Mulki Kassu  Miraj) alichaguliwa malkia wa Tanzania na  bara zima la Afrika.
Wateuzi wa ushindi huo hawakuangalia tu sura,  bali tabia, fikra, hamasa na msimamo wa kimaendeleo wa mhusika.  Washindani walitoka mataifa mbalimbali duniani.
“Ninataka kuiwakilisha nchi yangu na kuwasaidia wenye maisha magumu, niifanye dunia iwe mahali pazuri zaidi. Nafahamu si kazi rahisi ila nina hakika kila mmoja wetu akijumuika na mwenzake  mabadiliko mema zaidi yatafanyika. Tanzania ni nchi ya amani na ninaamini amani na mapenzi vyaweza kuongezeka katika jumuiya zetu.” – Kassu




Ali Sungura-mdhamini, Balozi Kallaghe, Malkia Kassu, Aisha Mohammed, Allen Kuzilwa- London 2013- pic by Said Surur

Kutoka kushoto ni mdhamini, Ali Sungura, Balozi wetu Uingereza , mheshimiwa Peter Kallaghe,  sahiba mkuu Aisha Mohammed na Afisa Ubalozi, Allen Kuzilwa
Malkia Kassu -2013

Malkia Kassu


Malkia Kassu with pals Andrew Matt and Ayesha Mohammed-pic by Jay Pedram

Malkia Kassu akipongezwa na marafiki, Andrew Matt na Aisha Mohammed.



Malkia with Diamond the Tanzanian star musician- 2013-pic by Kassu family
Malkia Kassu akiwa na mwanamuziki maarufu wa Bongo Fleva, Diamond karibuni.
Winner Malkia Kassu with friends Ayesha Mohammed and Andrew Matt


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Propellerads