YoungConciousâ„¢

Be Updated on the World of Sports, latest News and Entertainment Stories.

Propellerads

Breaking News

Translate

Welcome to Young concious .blogspot.com ==>>Feel free to leave your comment

Jumatano, 28 Agosti 2013

Wafahamu wachezaji wanaokaribia kusajiliwa na Tottenham.



Klabu ya Tottenham Hotspurs inakaribia kukamilisha usajili wa viungo Willian toka klabu ya Anzhi Makhachkhala na Erik Lamela toka As Roma .
William alikuwepo London hapo jana ambapo inaaminika amefanyiwa vipimo vya afya kabla ya uthibitisho wa usajili wake huku Lamela yeye akitarajiwa kutua jijini humo hii leo .
Hadi sasa Spurs imeshatumia zaidi ya pundi milioni 50 kuwasajili Roberto Soldado ,Nacer Chadli,Paulinho na Etienne Capoue  na usajili wa Willian pamoja na Lamela utaigharimu Spurs jumla ya paundi milioni 60.
Mfanyakazi wa Hoteli akipokea mizigo ya Willian.
Mfanyakazi wa Hoteli akipokea mizigo ya Willian.
Willian ambaye ni raia wa Brazil alianzai soka lake ndani ya klabu ya Shakhtar Donetsk ambako alijijengea jina akiwa na Wabrazil wenzie kama Fernandinho na Alex Texeira kabla hajajiunga na Anzhi Makhachkhala .
Willian akiwasili kwenye hoteli moja huko London tayari kukamilisha usajili na klabu ya Tottenham .
Willian akiwasili kwenye hoteli moja huko London tayari kukamilisha usajili na klabu ya Tottenham .
Erik Lamela amekuwa akiichezea klabu ya As Roma ambayo imemsajili toka Argentina ambapo inaaminika kuwa mkurugenzi mpya wa ufundi wa Spurs Branco Baldini ambaye aliwahi kuwa na nafasi hiyo ndani ya klabu ya As Roma amekuwa sehemu muhimu sana ya mchezaji huyo kuja Tottenham.
Erik Lamela ambaye Spurs inamsajili toka As Roma Ya Italia.
Erik Lamela ambaye Spurs inamsajili toka As Roma Ya Italia.
ERIK
WWWWILLIAN

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Propellerads