NI siku ya furaha kwa Kanye West! Kim
Kardashian amejifungua mtoto wa kike
Jumamosi asubuhi katika hospitali ya
Cedars-Sinai Medical Center, Los Angeles,
mtandao wa OMG umethibitisha.
Inasemekana Kardashian, 32, alikuwa na
West pembeni mwake wakati wa
kujifungua, kumkaribisha duniani binti
yao mwezi mmoja kabla ya muda
uliotarajiwa. Tarehe halisi ya kujifungua
ilitazamiwa kuwa Julai 11.
"Kim aliugua Ijumaa usiku na hatimaye
kupata mtoto mapema jumamosi," chanzo
cha hospitali kimeileza Us Weekly.
“Inafurahisha, wote wako katika hali
nzuri!"
Kanye West, 36, na Kim - wote wawili
wakiwa ndo mara ya kwanza kuwa
wazazi, wamekuwa wapenzi tangu Aprili
2012.
Desemba 30, 2012, West alitangaza
kwamba mpenzi wake alikuwa na mimba
wakati wa tamasha lake Atlantic City.
"Simamisha muziki na wote mpige kelele
kwa mama kijacho," alisema West
jukwaani akionyesha kidole kwa Kim
ambaye alikuwa mmoja wa watazamaji.
Translate
Jumapili, 16 Juni 2013
HATIMAYE KIM KARDASHIAN AJIFUNGUA MTOTO WA KIKE==>>Habari Kamili haPa<<==
About Young Concious
Soratemplates is a blogger resources site is a provider of high quality blogger template with premium looking layout and robust design. The main mission of templatesyard is to provide the best quality blogger templates.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni